Alhamisi, 25 Mei 2017

UUNDAJI WA MANENO

UUNDAJI WA MANENO
Maneno ya Kiswahili huweza kuundwa katika njia mbalimbali, kwa mfano; nomino inaweza kuundwa kutoka kwa nomino nyingine au hata kivumishi, aidha tunaweza kuunda nomino kutokana na vitenzi.
  1. Uundaji wa nomino kutokana na vitenzi.
Katika kuunda nomino kutokana na vitenzi, viambishi mbalimbali hutumika.Viambishi hivi hutokea  mwanzoni au mwishoni wa mzizi wa kitenzi kwa vyovyote vile mzizi lazima idumishwe.
Mifano ;
Vitenzi
nomino
l.a
Mlo,chakula,mlaji,mlafi,ulaji,ulafi
f.a
Mfu,kifo,ufu,maafa,ufuo
p.a
Mpaji,kipaji,kipawa
Pw.a
Pwani
Ny.a
Kinyesi,manyunyu
Nyw.a
Kinywaji,kinywa,mnywaji,unywaji
Ch.a
Uchao,macheo,mchana
Chw.a
Machweo
Kimbi.a
Mbio ,mkimbizi,mkimbiaji,ukimbizi,ukimbiaji
Hukum.u
Mhukumiwa,mahakama,hekima,hukumu,hakimu
Tembe.a
Mtembezi,matembezi,utembezi/utembeaji
Lip.a
Malipo,ulipaji
Lind.a
Mlinzi,ulindaji,ulinzi
Hukum.u
Hadimu,mhudumu,uhadimu,huduma
Andik.a
Maandishi,maandiko,mwandindishi,uandishi
Chor.a
Mchoraji,mchoro,uchoraji
Ogop.a
Mwoga ,woga
Oko.a
Mwokozi,wokovu,mwokovu,mkoaji
Takat.a
Mtakatifu ,utakatifu,mtakaso
Sem.a
Msemaji,usemaji,usemi
Simam.a
Usimamo,msimamizi,usimamizi
Lim.a
Mkulima,ukulima,kilimo
Chek.a
Mcheshi,ucheshi,kicheko
li.a
Mlio,kilio,mluzi,mlizi
Chez.a
Mchezo,mchezaji,uchezaji
Imb.a
Wimbo,mwimbaji,uimbaji

                                Matumizi
Tulicheza  vizuri sana ndipo timu yetu ikashinda.
T                                                               T
Ushindi wa timu yetu ilitokana na uchezaji mzuri.
N                                                        N
Jaji amemhukumu miaka minne gerezani.
Jaji ametoa hukumu ya kifungo cha miaka minne.wazazi hupata furaha kutokana na na utiifu mtoto.
Mtoto mwenye utiifu huwapa wazazi furaha.
Farasi aliyenona hawezi kukimbia.
Farasi mwenye unono hawezi mbio.
Mbio humshinda farasi mwenye unono.
Unono wa farasi humzuia kukimbia mbio.
  1. Uundaji nomino kutokana na nomino
nomino
nomino
mtu
Utu
Rafiki
Urafiki
Riziki
Ruzuku
Tabibu
Utabibu,tiba,matibabu/utibabu
Utungo
Mtunzi,utunzi
Mpenzi
Mapenzi,upendo,pendo
shujaa
Ushujaa
Elimu
Mwalimu,ualimu,alimu
kilimo
Mkulima ,ukulima
Mhadhiri
Uhadhiri,mhadhara,hadhira
siasa
mwanasiasa
salama
usalama
jengo
Mjenzi, ujenzi
  1. Kuunganisha nomino na nomino nyingine kuunda nomino ambatano
Nomino+nomino=nomino
Mja+mzito=mjamzito
Mwana+siasa=mwanasiasa
Mwana+hewa=mwanahewa
Mcha+Mungu=mchaMungu
Mwana+nchi=mwananchi
Miti+shamba=mitishamba
  1. Kuunganisha mikato ya nomino
Upungufu wa kinga mwilini-ukimwi
Chakula cha jiooni – chajio
Teknolojia ya habari na mawasiliano –teknohama
  1. Kuunganisha kitenzi na nomino
           Vunja +jungu=vunjajungu            pima+maji=pimamaji
          Pima+joto=pimajoto                     pima+mvua=pimamvua
  1. nomino kutokana na kivumishi

kivumishi
nomino
kitenzi
-refu
urefu
Refusha/refuka
-fupi
Ufupi
Fupisha/fupika
-eusi
weusi
©
-ekundu
wekundu
©
-erevu
werevu
erevusha

Matmizi
Werevu  wake ulimsaidia.             Ufupi wa Zakayo haukumfaa.
Hadhira ya watu imewasili.            Mhadhiri wetu amesafiri.
Fupisha kamba hiyo ili ikufae.       Ufupi wa kamba hiyo itakufaa.

Maoni 21 :

  1. Kongele,,,,, vyema sana

    JibuFuta
  2. Sifa kutokana na neno sali ni

    JibuFuta
  3. Adimika kitenzi yake ni gani

    JibuFuta
  4. Kitenzi kutokana na kivumishi karimu ni?

    JibuFuta
  5. Unda vitenzi kutokana na nomino zifuatazo;
    a) Hakimu
    b) Fitina
    c) Funza
    d) Ulezi
    Kindly assist

    JibuFuta
    Majibu
    1. Hukumu fitna funza lea

      Futa
  6. Unda kielezi kutokana na: 'enda'..tafadhali mbiombio🙏🙏

    JibuFuta
  7. Chapisho hili limeondolewa na msimamizi wa blogu.

    JibuFuta
  8. kivumishi cha ule zi

    JibuFuta
  9. Kivumishi kutokana na kitenzi

    JibuFuta
  10. Kitenzi Cha mlinzi

    JibuFuta