Alhamisi, 25 Mei 2017

MISINGI YA MANENO

MISINGI YA MANENO
  1. Mofimu
Mofimu ni dhana ambayo ni maana ambayo/zo huwakilishwa au kusetiriwa katika neno(mofu) ambalo tunaweza kulisikia linapotamkwa au kuliona linapoandikwa.

Dhana hii huweza kujitokeza kwenye mzizi au kiambishi
Mifano                   mofimu
Maria                     +msichana
                              +mmoja
                              +mtu/binadamu

Kuku                       +ndege
                                +mmoja/wengi
                                 +anayefugwa
                                + mayai
                               
      Ndege                      +kiumbe              +chombo                   
                                         +anayepaa           +kupaa
                                          +mmoja/wengi    +moja/nyingi
         Nitacheza          
                              Ni          +umoja
                                            +mtenda
                                            +nafsi ya kwanza
                               Ta         +wakati ujao
                               Chez     +mzizi
                                -a         +kiishio
Aina za mofimu
  1. Mofimu huru/mofimu za kimsamiati
Ni  mofimu zenye maana kamili hata bila kuambatanishwa na mofimu zingine.
Mofimu hizi hupatikana katika nomino,viwakilishi na hata vivumishi.mifano ya mofimu huru
  1. Katika nomino
Kuku              dawati             samaki           mama         baba
Shangazi         kabati              Kenya            Chaki         karatasi
  1. Katika viwakilishi
Mimi                sisi                 wewe              nyinyi        yeye
Wao       
  1. Mofimu katika vivumishi
Robo            bora                     nadhifu                hodari      jasiri
             Mofimu huru pia huitwa mofimu za kimsamiati.
  1. Mofimu tegemezi/ambata/funge
Ni mofimu ambazo haziwezi kujisimamia ,ni sharti zihusishwe na mofimu zinginezo.
Mifano;
Kiti  -ki+ti         mtume              mjamzito          walimoingia              mtu       madarasa
Changamoto       matunda            kipofu             gugumaji                   amenionea.

Uhainisho wa mofimu

  1. Mtoto
M          +umoja
toto       +mzizi
  1. Auma  
A           + ngeli
              + mtenda
              + nafsi ya tatu
              + umoja
Um         + mzizi
a             + kauli ya kutenda
  1. Hakukukumbuka.
Ha          +ukanusho
               +nafsi ya tatu
               +mtenda
Ku           +ukanusho
                +wakati uliopita
Ku           +nafsi ya pili
                +mtendwa
kumbuk   +mzizi
a             +kauli ya kutenda
bainisha mofimu katika sentensi hizi  na utaje kama ni huru ama tegemezi.
Amekimbia sana.                                     Kiti hiki ni kizito.
Tegemezi    huru                                   tege  tege   huru tege
fukia viazi hivyo                                                       endesha gari
huru         huru      tegemezi                                  tegemezi      huru
kaa        chini.                                     Amejipamba                 
huru      huru                                              tegemezi




  1. Viambishi
kiambishi ni kipashio cha kisarufi kinachoambatishwa au kinachofungamanishwa au kinachopachikwa katika mzizi wa neno ili kulipa neno maana mbalimbali.

Kiambishi ni mofu 
Aina za viambishi
  1. Viambishi awali-hupachikwa kabla ya mzizi wa neno.
  2. Viambishi tamati –hujitokeza /huja baada ya mzizi wa neno.
Mifano
Viambishi awali
mzizi
Viambishi tamati
maneno
m
geni
©
mgeni
Ki
geni
©
kigeni
U
geni
©
ugeni
U
geni
ni
ugenini
Ku
l
a
Kula
M
l
o
mlo
A
l
a
ala
Wa-me-ku
l
a
wamekula
©
li
a
lia
Hu
li
Liw-a
huliwa
M
li
o
mlio
Ki
li
o
kilio
li-li-li
li
li-a
lilililia
a-li-m
li
li-a
alimlilia

Matumizi ya viambishi vya masharti
  1. –nge
  • Huweza kutumiwa maradufu katika sentensi. Katika hali hiyo huonyesha kuwa vitendo vyote viwili havikutukia. Hata hivyo bado pana uwezekano wavyo kutukia. Kwa mfano;
Ningemwona ningemwambia. Katika mfano huu msemaji hakumwona anayerejelewa kwa hivyo hakumharifu alilopasa. Hata hivyo huenda akamwona baadaye na kisha kumwambia.
  • Katika hali kanushi, ni sharti vitenzi vyote  vinavyosheheni –nge lazima vikanushwe .hukanushwa kwa njia mbili;

  • Kwanza kutumia  ‘si’ baada ya kiambishi nafsi lakini kabla ya  -nge mfano
Nisingemwona nisingemwambia. Katika hali kanushi maana hubadilika na kuonyesha kuwa vitendo vyote vilitukia.
  • Aidha tunaweza kuzingatia nafsi husika pekee.
Singemwona singemwambia.
Ungeniharifu mapema ningekuletea.
Usingeniharifu mapema nisingekuletea.
Hungeniharifu mapema singekuletea.
  1. Ngali
Ikijitokeza maradufu kwenye sentensi, huonyesha vitendo vyote viwili havikutukia na hamna uwezekano wavyo kutukia kwa vyovyote vile.
m.f
Ningalimwona ningalimwambia .
Ukanushaji
Nisingalimwona nisingalimwambia.
Singalimwona singalimwambia.
Ikitumika mara moja kwenye sentensi huonyesha kuwa kitendo kiko katika hali ya kuendelea,m.f
Angali anacheza.        Mama angali anapika.   mtoto angali analia.
Kukanusha
                     Hachezi                    mama hapiki.                  Mtoto halii.
      Tanbihi : ‘nge’ na  ‘ngali’ havitumiwi katika sentensi moja
                 *ningemwona  ningalimwambia.

                                    Marejeleo
Nkwera, Fr. F. V. (2003), Sarufi, Fasihi na Uandishi wa Vitabu, Sekondari na Vyuo. Creative Prints Ltd: Dar es Salaam.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni