Alhamisi, 25 Mei 2017

VIPASHIO VYA LUGHA

 VIPASHIO VYA LUGHA
Ni vipengele ambavyo hushirikiana ili kujenga lugha.
Katika utaratibu huu vipashio vidogo vya lugha huungana ili kujenga vipashio vikubwa zaidi. Vipashio hivi ndivyo nguzo ya lugha na vinapoungana ndipo lugha hujengeka.
Katika kiwango cha chini zaidi kuna sauti ,nazo sauti huungana kujenga silabi ,silabi huunda maneno na maneno huungana kujenga sentensi.

sauti - silabi - neno          -     sentensi
silabi ni mapigo ya sauti katika neno.
Mifano
Aliondoka
a-li-o-ndo-ka (silabi tano)
ua
u-a (silabi mbili)
hufikirii
hu-fi-ki-ri-i(silabi tano)
muundo wa silabi katika sentensi
1 silabi ya irabu pekee
oa    o-a
ua    u-a
2 silabi za konsonanti na irabu
Soma  so-ma
3 silabi za konsonanti mbili na irabu
o-ndo-ka
4 silabi za konsonanti tatu na irabu
Mbweha  mbwe-ha
5 silabi za konsonanti pekee
Mchicha   m-chi-cha
Kelbu
Kuran

Maktaba

KIIMBO

KIIMBO
Namna ya kupaza na kushusha mawimbi ya sauti pale mtu anapotamka maneno.
Baadhi ya maneno hufanana kiimbo lakini kwa jinsi mawimbi ya sauti yanavyopanda na kushuka yakawa yana maana tofauti.
Mifano
Bara’bara-njia kuu
Ba’rabara-sawasawa
Wa’lakini-dosari
Wal’akini-ingawaje
Kata’kata-kukataa
Ka’takata-kugawa vipande
Kiimbo hutusaidia kubainisha lengo la msemaji wa lugha inayohusika, hivyo tunaweza  kutambua kama mzungumzaji anatoa maelezo ,anauliza swali,anaamuru ama anarai.
Aina za viimbo
Katika kusikiliza mazungumzo ya watu mbalimbali tunaweza kutambua kama mzungumzaji anatoa maelezo ,anauliza swali,anaamuru au anarai . tunatambua hivyo kutokana na namna kiimbo kinavyobadilika.
Vipo kama ifuatayo;
Kiimbo cha maelezo/taarifa
Kiimbo cha maulizo
Kiimbo cha mshangao
Kiimbo cha amri
Kiimbo cha rai
Sentensi za taarifa
Saparata anaandika barua.
Mama Resi anakoroga uji.
Sentensi za maswali
Dinda anaandika nini?
Mama Resi anakoroga nini?
Sentensi za rai/sentensi za maombi
Tafadhali nikorogee uji.
Niongezee tafadhali.
Sentensi za amri
Tembea haraka!
Funga mlango!
Kwenda kabisa!
Sentensi za mshangao

Muone Yule mrembo!

USEMI HALISI NA USEMI TAARIFA

USEMI HALISI NA USEMI WA TAARIFA
kauli zipo za aina mbili;
  1. kauli ya moja kwa moja kutoka kwa mnenaji hadi kwa msikilizaji jinsi ilivyo bila ya kufanyiwa mageuzi yoyote, kauli hii huitwa usemi halisi.
  2. Kauli inayopokewa kama maelezo ya yaliyosemwa pale awali na ambayo hufanyiwa mabadiliko fulani fulani ya hapa na pale, kauli hii huitwa usemi wa taarifa.
  1. Usemi halisi
Katika usemi huu yafuatayo huzingatiwa;
  • Alama za mtajo hutumiwa mwanzo na mwisho wa maneno yaliyosemwa.{“  “}
  • Kila baada ya kufungua ,sentensi huanza kwa herufi kubwa m.f
     “Hamjambo?”
“Shuhuda, tafadhali njoo tukatembee.”
  • Alama ya hisi,kiulizo,koma,nukta za dukuduku na kituo kikuu pia hutumiwa pamoja na alama za mtajo.Lazima zije kabla ya alama za kufunga. m.f
“Hunipendi?”
  • Msemaji mpya anapoanza kusema tunaanza aya  mpya maneno ya wazungumzaji wawili tofauti yasiwekwe katika aya moja.
Mwalimu akamhoji, “vipi?”

Mwanafunzi alijibu, “salama”
  • Kauli moja ikivunjwa katika vitengo, kitengo cha pili hata baada ya kuwekewa alama za kufungua ,neno lake la kwanza litaanza kwa herufi ndogo isipokuwa neno lilo likiwa nomino maalum.
  • Iwapo sentensi mpya inaanza baada ya msemaji kutajwa, herufi kubwa hutumika mwanzoni mwa hiyo sentensi mpya.
“Tukifika mjini Voi ,tutapumzika kwa muda wa saa moja.” Kiongozi wetu alisema. ”Baadaye tutaondoka na kwenda moja kwa moja hadi kisiwani Mombasa.”
“Haya! Habari ndiyo hiyo,” mwalimu alisema.
“Haya ,habari ndiyo hiyo.” Mwalimu alisema.
“Wiki ijayo tutakwenda kujionea mechi kati ya Harambee stars na Uganda Craines.” Rafiki yangu aliniambia.
“Mara nyingi binadamu uhitaji kutumia 'common sense.’ ”
  1. usemi wa taarifa
Hii ni ripoti kuhusu yaliyosemwa hapo awali. Yafuatayo huzingatiwa;
  • Alama za mtajo haziwekwi
  • Baadhi ya maneno yanaweza kubadilika lakini ujumbe uwe ni ule ule.
  • Alama za hisi na kiulizi hazitumiwi.
  • Aghalabu wakati uliopita ndo hutumika

                                              Mabadiliko



Usemi halisi
Usemi wa taarifa
                                                         viulizi
-ngapi?
Idadi
-ipi
Sifa/o-rejeshi/amba-rejeshi
-gani
o-rejeshi/amba-rejeshi/sifa
Je ,…?
Iwapo/ikiwa
…..je?
Jinsi/namna
Lini?
Wakati
Mbona?
sababu
Kwa nini?
Sababu
Vipi?
Jinsi/namna
                                                    Wakati/hali
-me-
-li-
-ta-
-nge-
Mwaka ujao
mwakani
sasa
Wakati huo
kesho
Siku iliyofuata
Jana
Siku iliyotangulia
                                            Nafsi
-ni-
-a-
-ku-
-ni-/m-

       
   
                                                                   viashiria
Hapa
Pale/hapo/alipokuwa
huku
Kule/huko/alikokuwa
huyu
Yule/huyo
                                                                      vihisishi
Tafadhali
alisihi
Salaala!
alishangaa
Nkt!
alifyonza
Uuuuwi!
Piga mayowe/npiga usiyahi
alhamdullilahi
alishukuru
Mungu wangu eeeh
aliomba
Arusi tunayo
shangilia
kwenda
Laani/puuza
Katika usemi wa taarifa matumizi ya maneno ‘kuwa’ na kwamba huruhusiwa  kwa mfano ;
“Mtoto ni mtoto, awe wa kiume au wa kike,” akasema mjomba,
Mjomba alisema kuwa…
Mjomba alisema ya kwamba mtoto ni mtoto awe wa kiume au wa kike.
“Mabasi hayapiti hapa siku hizi, kwa nini?” Neshboch aliuliza.
Neshboch alihoji/aliuliza/alitaka kujua sababu ya mabasi kutopita hapo katika siku hizo.
Madereva wakasema ,”Tutatii sheria za barabarani.”
Madereva walisema kuwa wangetii sheria za barabarani
“Leo nitakuonyesha kilichomtoa kanga manyoya,” Seki akamwambia Katango.
Seki alimwambia Katango  kwamba angemwonyesha kilichomtoa kanga manyoya siku hiyo.
“Afida , kwa nini  leo umechelewa darasani?” Kiranja akauliza.
Kiranja alitaka kujua sababu ya Afida kuchelewa darasani siku hiyo.
“Serikali ina mkono mrefu, hata ukijificha wapi utapatikana. ” Akakumbusha Chausiku .
Chausiku alikumbusha kwamba serikali ilikuwa na mkono mrefu na hata mtu angejificha popote angepatikana.
Mwanafunzi alisema kuwa angepita katika somo la Kiswahili.
“Nitafaulu katika somo la Kiswahili,”akasema mwanafunzi.
Mwanafunzi akasema,”Nitafaulu katika somo la Kiswahili.
Chifu aliwakumbusha kuwa ukimwi ulikuwa  ulikuwa ugonjwa hatari sana.
“Ukimwi ni ugonjwa hatari sana,”  chifu akawakumbusha.
Chifu akawakumbusha, “Ukimwi ni ugonjwa hatari sana.”
“Nawakumbusha kuwa ukimwi ni ugonjwa hatari sana.” Chifu akasema.
Kazimoto alishauriwa na kasisi kuwa  aache tabia za ulevi.
“Acha tabia ya ulevi,”kasisi akamshauri Kazimoto.
“Kazimoto  acha tabia ya ulevi,” kasisi akamshauri.
“Alimaliza fyu!”
Akamaliza yote
“Van persie , Van persie, goool!”
Alishangilia vanpersie alipofunga bao.
“Ni siku arubaini pekee ambazo zimebaki kabla ya Nineve kuangawizwa ikiwa hamtatubu dhambi zenu.” Jona akawatadharisha.
Jona aliwatadharisha watu kuwa siku arubaini pekee ndizo zilizobaki kabala ya Nineve kuangamizwa ikiwa awangetubu dhambi zao.
“wanipendeani mrembo?”
Alimuliza mrembo alikuwa anampendea nini.
"Anayenitesa si  adui yangu bali ni rafiki yangu tuliyojuana zamani,"Dzombo akasema.
Dzombo alisema kuwa aliyekuwa akimtesa hakuwa adui yake bali alikuwa rafiki yake waliojuana siku zilizopita.