Jumatatu, 12 Februari 2018

MHANGA NAFSI YANGU

MHANGA NAFSI YANGU
Mhanga nafsi yangu ni riwaya iliyoandikwa na Ammed Said Mohamed katika mwaka wa 2012,
kimechapishwa na  Longhorn publishers. Inazunguka katika maisha ya  Mhusika wake mkuu ambaye ni
Afida.
                           MAHUDHUI
                                 Usaliti
Usaliti unajitokeza kwenye wahusika wengi wakiwemo Afida anayesaliti ukoo wake na kukata minyororo
yao huku akilalamika kurudishwa nyuma na utegemezi wa motoni.Afida pia anamsaliti mpenziwe Shabaan
aliyemwandikia barua kila wakati tangu alipoenda peponi, Afida anakataa kujibu hizo barua,anadai kwamba
mapenzi yake kwa Shabaan yaliisha. Usaliti huu unampelekea Shabaan kuugua ugonjwa wa moyo na
hatimaye Shabaan anafariki. Vile vile Afida anawasaliti wazazin na walezi wake huku akisingizia kuwa
alishafika alikotaka, Afida na Shuhudia wanaisaliti dini yao,kulingana na dini yao hakufaa kuingilia ulevi
ambayo ni uasi wa kidini. Neshbosh bwanake Afida vile vile anasaliti ndoa yao na hatimaye kumfukuza
Afida nyumbani pake. Majirani wake Afida wanamsaliti kwa kumsingizi Afida kwamba alikuwa akimlelea
mtoto akiwa  mlevi na kumdhalilisha,  jambo hili linampelekea korti kutoa uamuzi wa kunyang’anyanywa
mtoto wake Dinda.
                               umaskini
Mataifa haya ya peponi wameyadhibiti masoko ya Motoni ambapo tunawaona wageni hawa wakija
Motoni na kununua matunda kwa bei ya chini. Hii inasababisha umasikini kwa Wamotoni kwanihawafaidiki
katika juhudi zao za kuzalisha mali.Kuhamia kwa Afida Peponi kulikuwa na msukumo wa kuasi ulitima na
kusaka mali Peponi.Tunaelezwa kuwa Motoni kulikumbwa na umasikini kiasi kwamba hakuna jambo njema
lolote
lililoweza kumea, kuwa au kukua katika nchi hii . Afida alilalamika Jinsi kule kutegemeana kwa ukoo wa
motoni kunavyozidisha umasikini hivi kwamba, mtu akionekana kufaulu, lazima ukoo ugawane mafanikio
yenyewe hata kabla hayajazaliwa. Eti mtu akifanikiwa kidogo, anakuwa mateka wa ukoo unaomnyofoa
nyama harakaharaka na kumegwa kila upande hadi mtu huyo abaki mifupa mitupu. Hii ni ishara tosha kuwa
Afida ametoka katika jamii iliyokumbwa na umasikini. Pia Katika maelezo ya Bi Sinangoa, tuanona kuwa
Afida
alilelewa kwa ukata kwani mara nyingi akienda kwa bibi huyu (Sinangoa) kupata angalau chakula. Wakati
mwingine Afida akipata kwa Singangoa hakukuwa na chakula, bibi huyu alikuwa akimtafutia angalau visenti
vidogo ilikununua chakula duni huko vijijini.Kazi aliyoifanya Bi. Mwamda baada ya kifo cha mumewe ni ishara
tosha ya umasikini.
                                          Ndoa
Kunazuka ndoa kati ya bwana Bawa na bibiye Marneti ambaye ni mmotoni, ndoa hii inadumu ila inasongwa
na tatizo la kupata mtoto, jambo hili linawapelekea wapange njama ya kumsawishi Afida kuwapa mtoto wake
Dinda. Afida anakataa jambo hili na kupelekea uhusiano wake na shangaziye Murneti kusambaratika.
Pia kunazuka ndoa kati ya Afida na Neshboch, ndoa hili limejawa na matatizo ya kila aina.Afida
anadhalilishwa na kuulizwa maswali ya kumdhalilisha na dadake Neshboch kwa jina la Sheshaiza, anamwuliza
siku ya harusi kama huko kwao Motoni amewahi kula vyakula vitamu kama vilivyo huko peponi, hatimaye
ndoa hii inavunjika Neshboch anapomfukuza bibiye, Afida anajipata katika ndoa ya pili kwa lengo la kupata
mtoto baada ya kunyanganywa pinda mtoto wake, anakuwa katika ndoa na saparata na wanapata mtoto kwa
jina mkombozi.
                                 Tamaa
Wamotoni wengi wana tamaa ya kwenda peponi, wengine wameishi kufa kwa tamaa hii. Mwandishi anasema
kuwa kuna wengine waliojaribu kukata jangwa la Sahara na kuishiwa kukumbwa na joto, kiu na kitaushi cha
maji mwilini na ambacho  mara humpoteza mtu uhai wake, jambo hili linawapelekea wamotoni kuhamia
Peponi wanakobaguliwa na kudhalilishwa, Afida pia anahamia peponi kwa tamaa ya kujiboresha kimaisha na
kuiacha umaskini uliomkumba.Tamaa ya utashi unampelekea Afida kuolewa na mzee Neshbosh aliyemzidi
umri.
                                   Ulevi
Ulevi inajitokeza kupitia kwa wahusika kama Afida, Neshboch, saparata na shuhuda, Afida na saparata
wanaathiriwa zaidi na ulevi. Punde tu Neshboch anapomfunza ulevi, ndoa yao inaingia msukomsuko. Baada
ya Afida kutalakiana na mumewa Neshboch anasingiziwa ulevi na majirani wake na hatimaye kunyang’anywa
mtoto wake Dinda, hapo ndipo Afida anajipagaza hilo jina  na hatimaye kuwa mlevi wa kupindukia. Ulevi huu
unampelekea Afida kuishiwa na pesa kwani baada ya talaka hakupata pesa tena  kutoka kwa Neshboch.
Hatimaye mtoto wake Mkombozi anapata katika harakati zake za kulewa anapoanza uhusiano na Saparata.
             Ukengeushi
Wamotoni  wengi wanapohamia Peponi huacha tamaduni zao na kuiga Wapeponi. Bi Marneti shangaziye
Afida alipokuwa Motoni alithamini utu, umoja na hakuwa na tamaa. Alipenda mapenzi safi yasiyo ya pesa,
kuuthamini ukoo wake na hakuropokwa ovyo. Alipohamia Peponi, alichukua tamaduni za huko na kutupilia
mbali tamaduni za Ki-Motoni hasa alipokata uhusiano na ukoo wake kiasi cha kumdhulumu Afida aliyekuwa
kama mtoto wake.Shuhuda rafikiye Afida aliyetoka Afrika aliiga Uzungu kwa mavazi, ulevi, hulka na hata
lugha.Alivalia vijiguo vilivyomuacha tuputupu kama anavyodai Afida. Alivuta sigara ambayo inadaiwa kuwa
haikumtoka mdomoni . Alienda kwenye mabaa na kushiriki ukware uliomfanya aambukizwe ukimwi. Mambo
haya yote Shuhuda aliyaiga kutoka kwa Wapeponi ambapo hata Afida hakuamini kuwa ni Shuhuda
aliyemfahamu kule Motoni. Shuhuda anasisitiza kuwa iwapo mwanamke yeyote anagependa mambo yake
yamwendee vyema kule Peponi,hakuwa na budi ila kuonyesha mwili wake .
                              Ubaguzi
Abiria waliokuwa kwenye basi na Afida walimtazama kwa chuki naye aliwapa tabasamu la kudanganya
.Moyoni alielewa chuki ya hao abiria hasa bibi mmoja aliyezoea kupanda naye basi lilo hilo kila siku, kwamba
ilikuwa ya kubaguliwa yeye kwani hakuwa Mpeponi. Chuki ilisheheni hata shuleni alikoenda Afida kwani
alidhaniwa kuwa na fahamu ya chini kuliko wanafunzi wote waliokuwamo darasani. Anasisitiza kuwa
wanafunzi walimtenga na kumuona dude tu. pia dadake Neshboch, Shesheiza anamwuliza Afida maswali ya
kumbagua. Anamwuliza kwamba kama huko kwao pia wanakula vyakula vitamu jinsi vilivyo peponi.
                           SIFA ZA AFIDA
                              Msomi
Afida anapoelekea peponi anajiunga na chuo cha peponi huku akigharamiwa na bwana Bawa na bibiye
Murneti. Anasoma kwa bidii mpaka anapita somo fulani na kusemekana kuwa Afida ndiye Mmotoni wa
kwanza kupita kiasi hicho baada ya miaka kumi na mitano, japo Afida hamalizi shule wala kufuzu anaonyesha
nia ya kutaka kuendeleza masomo yake japo anakumbwa vizingiti kama kuolewa na bwana Neshboch.
                             Msaliti
Afida anayasaliti mapenzi yake na Shabaan ingawa alimwahidi kwamba angeasi mapenzi hayo, pia anasaliti
walezi wake kama Sinangoa na Mamake kwa kutoshulika na wao anapofika peponi, anaandikiwa barua
nyingi na wamotoni ambayo anayapuuza Afida.
                           Mkengeushi
Afida pamoja na Shuhuda wanauacha utamaduni wa motoni na kuiga utamaduni wa Peponi ,hili linadhihirisha
katika nguo anazong’ara Afida, na ulevi wa kupindukia na hata hulka zake.


                            Mwenye bidii
Anapoolewa na Saparata anajitahidi kufanya kazi kwa bidii ili ahikimu matakwa ya mtoto wao Mkombozi, ili
ni baada ya Saparata kukataa kutoa msaada kwa mtoto wake Mkombozi.
                           Mpenda anasa
Afida anapopata talaka kutoka kwa mzee Neshboch  maisha yake yanachukua mkondo upya, anaanza
kujiingiza katika vitendo vya anasa, hili linaanza pindi anaponyang’anywa mtoto wake dinda. Hajiheshimu
tena anauza mwili wake kingono katika harakati za kupata pesa za kustahihisha mahitaji yake. Anaenda
kwenye baa na kutamka wazi kwamba anataka mtoto na angependa apewe, maisha yake Afida yanachukua
mkondo upya  asiwe afida aliyedhaniwa kuwa na msimamo dhabiti.


                              Mlevi
Afida anaponyanganywa mtoto wake Dinda baada ya kusingiziwa na majirani yake kuwa mlevi, anajiingiza
katika ulevi wenyewe huku maisha yake yanazoroteka katika ulevi.
                     Mwenye msimamo dhabiti
Anapoambiwa na bwana Bawa ba bibiye Murneti awapee mtoto wamtunzie anakataa wazo hilo na
kutafautiana na mumewe na shangaziye. Pia yakrobich anapomtakia uhusiano wa kimapenzi anakataa na
kuona isiyokuwa na maana.

Maoni 2 :

  1. Jadili Tamathali za usemi na taswira katika riwaya ya Mhanga Nafsi yangu .

    JibuFuta